Shule ya Wasichana Hazrat Zainab (s.a.) iliyopo Kigamboni, Dar es Salaam, imeandaa darasa la Tafsiri ya Qur’ani Tukufu pamoja na maombolezo ya Imam Hussein (a.s.), ambapo washiriki walijadili athari za vita vya kisaikolojia katika kudhoofisha fikra, imani na maadili ya vijana.
